WorldCat ni jina la hazinadata kubwa zaidi duniani kuhusu vitabu vinavyopatikana katika maktaba elfu kadhaa kote duniani.
WorldCat ni kifupi cha "world catalogue" yaani orodha (ya vitabu) ya kimataifa.
Ilianzishwa mwaka 1967 wakati maktaba za jimbo la Ohio, Marekani ziliungana kuunda taasisi ya "Ohio Computer Library Center" (OCLC) kwa shabaha ya kupeana habari za vitabu vilivyopatikana katika maktaba za vyuo 54 vya Ohio.
Tangu mwaka 1978 maktaba za majimbo mengine ya Marekani yalikubaliwa na jina kubadilishwa kuwa "Online Computer Library Center".
Tangu mwaka 2002 kila maktaba duniani inaweza kujiunga na OCLC. Mwaka 2019 kulikuwa na maktaba wanachama 17,983 katika nchi 123 tofauti.
Ukitafuta kitabu kwenye WorldCat itakupa majina ya maktaba wanachama ambamo kitabu hicho kinapatikana. Kama hakuna maktaba iliyo karibu yenye kitabu hicho unaweza kuazima kitabu (karatasi au online) kama maktaba yako ni mwanachama ya WolrdCat na kukubali kuazima kutoka maktaba nyingine.
WolrdCat inatoa pia nafasi ya kupata habari zinazohitajika kwa dondoo kwa kubofya "Cite/Export" (copy a citation).
(zote ziko Nairobi kama mahali pengine hapatajwi)
(zote ziko Dar es Salaam kama mahali pengine hapatajwi)
(zote ziko Kampala kama mahali pengine hapatajwi)
|date=
(help)