Bioanwai (pia baioanwai; kwa Kiing. biodiversity) ni dhana ya biolojia inayoleenga kueleza wingi wa anwai za spishi za kibiolojia katika mazingira fulani, pamoja na wingi wa jeni katika mimea na wanyama wa eneo fulani.
Bioanwai ni muhimu kwa sababu viumbehai wote wanategemeana kwa namna fulani.
Bioanwai ni muhimu kwa binadamu kwa namna nyingi. Mimea hutoa oksijeni na kusafisha hewa chafu. Mimea hutoa pia chakula, kivuli, vifaa vya ujenzi, dawa na nyuzi za nguo na karatasi. Mizizi ya mimea inapunguza mmomonyoko na mafuriko. Mimea, fungi na wadudu hutunza rutuba ya udongo na kusafisha maji. Kadri bioanwai inavyopungua, mifumo hiyo inaharibika.
Mfano ni matumizi ya kemikali katika kilimo yaliyolenga wadudu wanaoharibu mazao; lakini dawa hizo zunaathiri wadudu wote; katika nchi zenye matumizi makubwa ya dawa hizo idadi ya wadudu kwa jumla imepungua na kuhatarisha kustawi kwa mimea mingi pamoja na kilimo cha matunda.
Kuelewa na kutunza bioanwai ni shabaha muhimu katika hifadhi ya mazingira.