Majira yaligawiwa kwa miezi minne yenye siku 30. Hii miezi 12 hapo awali ilitajwa kwa namba lakini baadaye ilijulikana pia kwa majina ya sherehe zake kuu. Kila mwezi uligawanywa katika miongo mitatu ya siku 10.
Mwaka mfupi
Mwaka huo ulikuwa mfupi kuliko mwaka wa jua kiasi cha karibu robo siku. Kalenda ya Wamisri ilipoteza karibu siku moja kila baada ya miaka minne kulinganishwa na Kalenda ya Gregori. Hali hiyo ilitambuliwa kama hasara, lakini majaribio ya kusahihisha kasoro kwa kuongeza siku ya sita ya nyongeza kila baada ya miaka minne yalishindikana kutokana na upinzani kwa viongozi wa dini.
Kalenda ilianzishwa mapema wakati wa milenia ya 3 KK. Wataalamu wa Misri ya Kale walitambua kwamba nyota ya Shira (Sirius) ilianza kuonekana angani kila mwaka wakati huohuo kama kutokea kwa mafuriko ya Mto Naili. Hivyo tarehe ya kuonekana kwa Shira mnamo 19 Juni ilikuwa siku ya mwaka mpya wakati kalenda ilipoanzishwa; ila tu, kutokana na ufupi wa mwaka wa Kimisri, Shira ilianza kutokea kabla ya siku ya mwaka mpya.
Matumizi baada ya Misri ya Kale
Tangu masahihisho yaliyofanywa chini ya Kaisari Augusto, kalenda iliendelea sambamba na Kalenda ya Juliasi ya Waroma. Pia baada ya uvamizi wa Waarabu na kuenea kwa Uislamu iliendelea kutumiwa na Kanisa la Kikopti kwa kupanga liturgia na sikukuu zake.
Pia wakulima wa Misri, wakiwa Wakristo au Waislamu, waliendelea kutumia kalenda hiyo kwa kukadiria kazi zao zilizotegema majira ya mafuriko ya mto Naili.
Grafton, Anthony Thomas n.k. (1985), "Technical Chronology and Astrological History in Varro, Censorinus, and Others", The Classical Quarterly, Vol. XXXV, No. 2, ku. 454–465.
Krauss, Rolf n.k., mhariri (2006), Ancient Egyptian Chronology, Handbook of Oriental Studies, Sect. 1, Vol. 83, Leiden: Brill.
Luft, Ulrich (2006), "Absolute Chronology in Egypt in the First Quarter of the Second Millennium BC", Egypt and the Levant, Vol. XVI, Austrian Academy of Sciences Press, ku. 309––316.
Neugebauer, Otto Eduard (1939), "Die Bedeutungslosigkeit der 'Sothisperiode' für die Älteste Ägyptische Chronologie", Acta Orientalia, No. 16, ku. 169 ff. Kigezo:In lang
O'Mara, Patrick F. (January 2003), "Censorinus, the Sothic Cycle, and Calendar Year One in Ancient Egypt: The Epistemological Problem", Journal of Near Eastern Studies, Vol. LXII, No. 1, Chicago: University of Chicago Press, ku. 17–26Check date values in: |date= (help).
Spalinger, Anthony (January 1995), "Some Remarks on the Epagomenal Days in Ancient Egypt", Journal of Near Eastern Studies, Vol. 54, No. 1, ku. 33–47Check date values in: |date= (help).
Calendrica Includes the Egyptian civil calendar with years in Ptolemy's Nabonassar Era (year 1 = 747 BC) as well as the Coptic, Ethiopic, and French calendars.
Civil, ver. 4.0, is a 25kB DOS program to convert dates in the Egyptian civil calendar to the Julian or Gregorian ones